|
UTARATIBU WA KUFUNGUA SHULE ZA MAFUNZO YA UDEREVA: Shule za udereva zinasimamiwa na sheria inayoitwa “THE DRIVING SCHOOL ACT CHAPTER 163 OF LAW OF 1965 R.E 2002”. Sheria hii inaelezea wazi kwamba Mkuu wa Jeshi la Polisi (I.J.P) ndiye mwenye mamlaka ya kusajili shule zote za udereva Tanzania. Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani amekasimiwa madaraka hayo na I.J.P, hii ni pamoja na kubuni mikakati ya uboreshaji wa shule hizo za udereva ili kukidhi utoaji wa taaluma bora.
|
