Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikata utepe kuzindua huduma ya X-ray katika Hospitali kuu ya Polisi iliyopo barabara ya kilwa, kurasini jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikagua machine ya miozi (x-ray) mara baada ya kuzindua huduma hiyo katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dare s salaam.
Kikundi cha sanaa cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kusherehesha hafla ya uzinduzi wa huduma ya x-ray katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dar es salaam
| Traffic Junior Patrol |
|
UTARATIBU WA UVUKAJI BARABARA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI ZILIZOPO KANDOKANDO MWA BARABARA (JUNIOR PATROL)
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) SACP. MOHAMED R. MPINGA akizindua rasmi utaratibu wa uvukaji Barabara kwa wanafunzi wa shule za msingi (Junior Patrol) Kutokana na ongezeko la ajali za barabarani zinazotokea mara kwa mara hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi zilizopo kandokando mwa barabara, Jeshi la polisi, kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani (T) , limebuni utaratibu wa wanafunzi kuvushana wao kwa wao kwa kutumia vibao maalum. Mfumo huu umefanikiwa kwa kiasi kikubwa nchini Malawi na unajulikana kwa jina la ‘SCHOLAR PATROL’, na umepunguza ajali za wanafunzi kwa kiasi kikubwa,hivyo kikosi cha usalama barabarani kimeona mfumo huo ni mzuri kuigwa hapa nchini. Baada ya wanafunzi wa baadhi za shule za Dar Es Salaam kupata mafunzo ya zoezi hili, mfumo huu ulizinduliwa rasmi na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) SACP. MOHAMED R. MPINGA, tarehe 29.01.2011 katika Barabara ya Ally Hassan Mwinyi. Hivyo basi zoezi hilo limeshaanza kwa shule 12 za Mkoani Dar Es Salaam na Shule 2 za mkoani Mbeya. Lengo ni zoezi hili lisambae shule zote zilizokuwa kandokando mwa barabara katika Mikoa yote Tanzania Bara. LENGO.
VIFAA VINAVYOTUMIKA KWENYE MPANGO HUO.
Jacketi la kuakisi mwanga linavyoonekana kwa nyuma linalovaliwa na mwanafunzi anayewavusha wenzake. UTARATIBU WA UVUSHAJI WANAFUNZI ((JUNIOR PATROL) Baada ya wanafunzi kupata mafunzo ya utaratibu huu wa Junior Patrol kutoka Jeshi la Polisi.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Mbuyuni na kumbukumbu za Jijini Dar Es Es Salaam wakipata maelekezo ya utaratibu wa Junior Patrol toka Jeshi la Polisi.
Katika maeneo ambayo hakuna zebra wanafunzi hao watatakiwa wasimame sehemu ambayo ni salama kwa ajili ya kuwavushia wenzao .
|