Saturday, May 19, 2012

Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikata utepe kuzindua huduma ya X-ray katika Hospitali kuu ya Polisi iliyopo barabara ya kilwa, kurasini jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikagua machine ya miozi (x-ray) mara baada ya kuzindua huduma hiyo katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dare s salaam.

Kikundi cha sanaa cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kusherehesha hafla ya uzinduzi wa huduma ya x-ray katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dar es salaam

Kusajili Shule za Udereva

USAJILI WA MKUFUNZI  WA SHULE ZA UDEREVA

 

  • Mwombaji awe na umri wa  miaka 21 na kuendelea
  • Awe na leseni halali ambayo inamruhusu kuendesha daraja analotaka kufundisha na pamoja na hati ya ushindi  (certificate of competence.)
  • Mwombaji anatakiwa kwenda Ofisi ya Mkuu wa Polisi, Usalama Barabarani (RTO) Mkoa husika, au aende  moja kwa moja Ofisi ya Kamanda Polisi, Usalama Barabarani (T). Na kutakiwa kujaza form ya  kuomba kujaribiwa/kutahiniwa.
  • Atatahiniwa na Mkaguzi wa magari/mtahini wa madereva. Mtihani huo unalenga maeneo makuu yafuatayo:-
  • Kupima uwezo wa kuendesha na kulimudu gari awapo barabarani.
  • Uelewa wa Sheria ya Usalama Barabarani na  kanuni za njia (highway code) pamoja na matumizi ya alama za barabarani.
  • Uwezo wa kutoa maelekezo kwa wanafunzi wakati wa mafunzo kwa vitendo.

 

  • Mwombaji atakayefaulu atapewa cheti cha ushindi iwapo atashinda.
  • Mtahini atajaza fomu kuthibitisha uwezo wa mwombaji.
  • Mtahiniwa atajaza fomu kwa ajili ya kuomba kusajiliwa.
  • Usajili utatolewa na Ofisi ya Kamanda wa  Polisi, Usalama Barabarani (T).

 

Makosa ambayo mwalimu wa madereva anaweza kunyang’anywa leseni.

  • Iwapo atakuwa ameonywa na kurudia makosa yaleyale aliyoonywa
  • Iwapo atakuwa ameadhibiwa mara mbili au zaidi kwa kosa lilelile.
  • Iwapo atapoteza sifa ya kumiliki leseni ya Udereva.
  • Iwapo atafutiwa leseni na Mahakama.

 

Ikumbukwe kwamba leseni hii itakuwa halali hadi hapo itakapositishwa na   Jeshi la Polisi, au iwapo atakiuka Sheria  ya Usalama Barabarani.