
Askari wa Polisi Wanamaji wakiwa kwenye mafunzo ya kuzuia ugaidi (Comprehensive Maritime Security Manda Bay, Kenya). Mafunzo haya yanatolewa na serikali ya Marekani kuwajengea uwezo Askari na baadaye kuwa wakufunzi wa wengine. Mafunzo yanayotolewa ni:-
Comprehensive Maritime Security
Maritime Port and Harbors Security
Advanced Outboard Motor Maintenance
Maritime Interdiction of Terrorism
Kikosi cha Polisi Wanamaji Kina seksheni nne ambazo ni:-
Nahodha (Navigation)
Ufundi (Engineering)
Uzamiaji ( Scuba diving)
Ubaharia (Seamanship)

Nahodha D.5815 S/SGT Maximillian akiwa katika shughuli ya kuongoza meli wakati wa doria ndani ya Bot PB. 20 Mamba.

Fundi A/INSP Bakari Fumbwe akirekebisha
mitambo wakati wa doria kwenye Boti PB. 20 Mamba
Boti mpya Fibre glass PB.21 Ulinzi Shirikishi ikiwa kwenye ghati tayari kwa doria. Boti hii hufanya doria Territorial waters

Boti PB. 20 Mamba ikiwa kwenye ghati. Boti hii hutumika kwa doria kwenye Territorial waters.

Mashua 2 za Fibre Glass tulizopewa na Serikali ya Marekani ambazo zitafanya kazi ya kuzuia uhalifu kwenye mwambao wa bahari ya Hindi. Boti hizi ziko saba na zimegawiwa kama ifuatavyo:-
Mwanza – 2
Dar es Salaam – 2
Zanzibar – 2
Tanga – 1
Kwa vile nia ya Kikosi ni kukifanya kiwe cha kisasa kwa kutumia teknolojia za kisasa, tumekuwa tukitoka taratibu kwenye teknolojia ya zamani na kuanza kutumia Computer kwa ajili ya utunzaji kumbukumbu za askari na sasa tuna data base ya askari wote wa Polisi Wanamaji Tanzania.

INSP Naanjela – Mtaalamu wa IT akiwa kazini

Katibu Muhtasi Ndugu PeninaNdembo akiwa kazini

NDUGU JOSEPH O ABACH
Mhasibu wa Kikosi Ndugu Joseph O. Abach ambaye hushughulikia mambo yote yahusuyo fedha.

ASP MOHAMED
Kikosi hiki kina Idara pia ya Intellijensia ambayo inaongozwa na ASP Mohamed. Kazi kubwa ni kukusanya taarifa za kiitelijensia na kuzitumia wakati wa kufanya doria. Doria hizi zinatakiwa kuwa zenye malengo.
Kikosi cha Wnamaji Tanzania ndicho hushughulikia vituo vingine vya Wanamaji kwenye mambo ya kiufundi. Askari NO. E.7216 P.C Deogratias Mihanda ndiye mtunza stoo ya kikosi, huingiza na kutoa vifaa vyote ambavyo vinatakiwa mikoani.
Ajira katika Kikosi cha Polisi Wanamaji wanatakiwa wawe na ufahamu wa maeneo yafuatayo:
Ubaharia na upigaji mizinga (seamanship and gunnery)
Unahodha (Navigation)
Ufundi wa meli (Marine Engineering)
Uzamiaji (Scuba diving)
Umeme (Electrician)
Utaalamu wa Rada (Radar technicians)
Utaalamu wa kutuma Rada (Radar Operations)
Upakaji rangi wa meli (Painting)
Upishi (Catering)
Walikuwa njiani kutoroka kupitia mpaka wa Namanga.FBI watua kuchunguza. Jeshi la Polisi mkoani Arusha , linawashikilia kwa mahojiano watu wenye asili ya kiarabu wanaotuhumiwa kulipua bomu kanisa katoliki jijini Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine 59 kujeruhiwa. Kwa upande mwingine askari wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), wamewasili mjini Arusha jana asubuhi kwa ajili ya kuongeza nguvu ya kuwasaka watu waliohusika na mlipuko wa bomu katika kanisa la Parokia ya Joseph Mfanyakazi Olasite.
Maoni ya Mhariri, anasema kuwa kufuatia kauli iliyotolewa na Mbunge wa Iramba Mashariki, Tundu Lissu, kwamba katika tukio la bomu jijini Arusha, serikali ndiyo inapaswa kulaumiwa kwa vile ndiyo chanzo cha chokochoko za udini nchini, kauli ambayo imelaaniwa vikali na haikupaswa kutolewa hasa kwa kiongozi kama yeye kutokana na kauli hiyo kutokuwa na lengo la kuchangia au kusaidia kutafuta ufumbuzi wa tatizo bali kuzidisha tatizo lenyewe
Watu watano wanashikiriwa mkoani Ruvuma kwa tuhuma mbalimbali za uhalifu likiwamo la kukutwa na risasi pamoja na mikia miwili ya tembo.
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Matenga, kata ya Ikuwo, wilayani Makete wametakiwa kuelewa dhana ya utii wa sheria bila shuruti inayotekelezwa na Jeshi la Polisi nchini ili kuondokana na athari zinazotokana na kukaidi kutii sheria.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga Costantine Massawe, amewataka watu wanaojihusisha na biashara za dawa za kulevya, kuwaonea huruma wakazi wenzao wa Jiji la Tanga kutokana na madhara ya kiafya wanayoyapata baada ya kujiingiza kwenye matumizi yake. Ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya kukamata kilo 178 za bangi na kilo 52 za mirungi kwa waandishi wa habari mkoani humo.
Upelelezi wa kesi inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wifred Lwakatare na Ludovick Joseph, umekamilika na jalada lake litapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kwa hatua zaidi.
Jeshi la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kukusanya kiasi cha zaidi ya Shilingi Milioni 825 kutokana na makosa madogo madogo ya barabarani kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Mwinyihaji Makame amesema ushiriki wa wananchi katika Ulinzi Shirikishi kupitia Polisi Jamii umeleta mafanikio katika kupunguza vitendo vya uhalifu nchini