Saturday, May 19, 2012

Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikata utepe kuzindua huduma ya X-ray katika Hospitali kuu ya Polisi iliyopo barabara ya kilwa, kurasini jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Said Mwema akikagua machine ya miozi (x-ray) mara baada ya kuzindua huduma hiyo katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dare s salaam.

Kikundi cha sanaa cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kusherehesha hafla ya uzinduzi wa huduma ya x-ray katika hospitali kuu ya Polisi barabara ya kilwa kurasini jijini Dar es salaam

Mwenyekiti wa SARPCCO ambaye pia ni Kamishina wa Polisi wa Afrika kusini Luteni Jenerali N.S. Mkhwanazi akipokelewa na Kamishina wa Operesheni, CP. Paul Chagonja katika uwanja wa ndege kimataifa wa Mwalimu Julius kambalage Nyerere mara baada ya kuwasili nchini.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema kushoto akimpokea mgeni wake Mwenyekiti wa SARPCCO ambaye pia ni Kamishina wa Polisi wa Afrika kusini Luteni Jenerali N.S. Mkhwanazi alipowasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kwa ziara ya kikazi hapa nchini.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Pereira Silima akimkaribisha Mwenyekiti wa SARPCCO ambaye pia ni Kamishina wa Polisi wa Afrika kusini Luteni Jenerali N.S. Mkhwanazi alipowasili ofisini kwake Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa SARPCCO ambaye pia ni Kamishina wa Polisi wa Afrika kusini Luteni Jenerali N.S. Mkhwanaz akiwa na Mwenyeji wake Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema, Kamishina wa Utawala na Fedha pamoja na Kamishina wa operesheni wa Jeshi la Polisi wakiwa katika mkutano na wandishi wa habari.

UTII WA SHERIA BILA SHURUTI

RASIMU YA ANDIKO LA MPANGO WA KAMPENI YA UTII WA SHERIA ZA NCHI BILA SHURUTI
UTANGULIZI

Jeshi la Polisi Tanzania kwa kushirikiana na wadau wakewa HAKIJINAI, limeanzisha kampeni ya kuiwezesha jamii kutambua umuhimu wa utii wa sheria za nchi na taratibu za jamii bila shuruti.
Kampeni hii ni moja ya juhudi zinazolenga kuboresha maadili ya jamii kama msingi wa maendeleo yanayozingatia usalama, amani na utulivu ambazo ni nguzo za ustawi wa kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.
Msingi wa kampeni hii unalenga kuongeza ari na moyo wa uzalendo unazingatia uwajibikaji katika harakati za kujiletea maendeleo bila kuvuja sheria za nchi.
LENGO KUU
Kuongeza kiwango cha utii wa sheria za nchi bila shuruti jambo ambalo litasaidia kupunguza uhalifu na matumizi ya shuruti katika usimamizi ya utiifu wa sheria za nchi. Utaratibu huu pia utasaidia kupunguza gharama katika oparesheni za kupambana na uhalifu.

Aidha, utii bila shuruti utasaidia kupunguza msongamano wa kesi mahakamani na idadi ya wafungwa/mahabusu wanaotakiwa kuhudumiwa na Idara mbalimbali kwa kodi za wananchi.

 

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IJP Said A. Mwema akipita juu ya moto jana jijini Dar es Salaam baada ya kupata mafunzo kutoka taasisi ya Peak Perfomance ya kujengewa ujasiri na uwezo wa ujiamini zaidi katika utendaji kazi wa kila siku

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini Kamishna wa Polisi, Robert Manumba akipita juu ya moto jana jijini Dar es Salaam baada ya kupata mafunzo kutoka taasisi ya Peak Perfomance ya kujengewa ujasiri na uwezo wa ujiamini zaidi katika utendaji kazi wa kila siku.

Kamishna wa Utawala na Fedha, CP Clodwig Mtweve akipita juu ya moto jana jijini Dar es Salaam baada ya kupata mafunzo kutoka taasisi ya Peak Perfomance ya kujengewa ujasiri na uwezo wa ujiamini zaidi katika utendaji kazi wa kila siku

 

 

We have 75 guests online

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IJP Said A. Mwema akiwa na baadhi ya maofisa wakuu wa Polisi kwenye makundi jana jijini Dar es Salaam wakati ya kupata mafunzo kutoka taasisi ya Peak Perfomance ya kujengewa ujasiri na uwezo wa ujiamini zaidi katika utendaji kazi wa kila siku.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IJP Said A. Mwema akiwa  katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wakuu wa Polisi mara baada ya zoezi la kujiamini kupita juu ya moto jana jijini Dar es Salaam walipokua wakipata mafunzo kutoka taasisi ya Peak Perfomance ya kujengewa ujasiri na uwezo wa ujiamini zaidi katika utendaji kazi wa kila siku.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiongozwa na kikosi cha bendera cha Chuo Cha Polisi Moshi wakati akiingia kufungua Mkutano Mkuu wa Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi uliofanyika Mjini Moshi, Machi 2012.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kama ishara ya kuzindua rasmi utekelezaji wa Mpango wa Maboresho ndani ya Jeshi la Polisi katika Chuo Cha Polisi Moshi wakati alipokwenda kufungua Mkutano wa Maofisa waandamizi wa Jeshi hilo, Machi 2012.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama (CDF) Jenerali Devis Mwamunyange akitoa mada katika Mkutano Mkuu wa Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mkutano wa Chuo cha Polisi Moshi Machi mwaka huu.

 

Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi wakisikiliza mada kwa umakini katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Polisi Moshi.