Main Menu
Useful Links
| Tahadhari za Usalama |
| Polisi Jamii |
| Vifungu vya Sheria |
| SMS & CALLS |
Who's Online
We have 1 guest onlineLogin Form
|
UJUMBE KUTOKA KWA INSPEKTA JENERALI WA POLISI Je una taarifa za Uhalifu au Wahalifu?? Ewe mwananchi usisite kutoa taarifa Polisi kwa kufika kituoni na kutuletea taarifa ama kwa njia mbalimbali za mawasiliano ambazo Jeshi hivi sasa limeziboresha ili kurejesha ukaribu na uaminifu kati ya jamii na Jeshi la Polisi Waweza kutuletea taarifa ya Uhalifu ama Wahalifu kupitia simu yako ya mkononi kwa kutuandikia ujumbe mfupi (SMS) na kuituma kwenda Namba 111/112 au ukaituma kwenye namba ya mkoa uliopo karibu nawe. Ama pia waweza kutuandikia taarifa ulizo nazo hapa hapa kwenye mtandao wetu kwa kubonyeza ukurasa wa malalamiko/maoni. NB: Namba za kutumia sms mikoa yote bara na visiwani tazama katika ukurasa wa Wasiliana Nasi
"Amani, utulivu na usalama wa raia na mali zao ni mhimili wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Taifa lolote. Kupambana kwa wimbi la uhalifu na kuzorota kwa usalama wa raia huathiri mfumo mzima wa maisha ya jamii na kudhoofisha nguvu ya jamii hiyo katika kujiletea maendeleo." Na. Said Mwema - Inspekta jenerali wa Polisi - Tanzania
|
|







